FAHAMU FAIDA ZA KUMILIKI KIWANJA CHENYE HATI MILIKI

Unapokua unamiliki kiwanja/eneo ni muhimu kuwa na HATI miliki kwasababu kuna Faida mbalimbali zinazotokana na mtu kuwa na hati miliki 👇

𝐅𝐀𝐈𝐃𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐔𝐀 𝐍𝐀 𝐇𝐀𝐓𝐈𝐌𝐈𝐋𝐈𝐊𝐈

1)𝐔𝐓𝐀𝐌𝐁𝐔𝐙𝐈 wa kisheria kuwa yeye ni mmiliki halali wa kipande hiko cha 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈.

2)𝐇𝐀𝐓𝐈 𝐌𝐈𝐋𝐈𝐊𝐈 yako Inaweza kutumika kama dhamana katika uombaji wa mikopo benki na taasisi za kifedha. (Hivyo inaweza kukuinua kiuchumi)

3)Kupunguza /Kuondoa 𝐌𝐈𝐆𝐎𝐆𝐎𝐑𝐎 na majirani zako na pia usumbufu pindi unapotaka kuiuza ardhi hiyo.
Hivyo 𝐏𝐀𝐍𝐆𝐀, 𝐏𝐈𝐌𝐀 ardhi yako na umiliki 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐄𝐑𝐈𝐀 kwa usalama na maendeleo ya baadae.

4)Kuongeza 𝐓𝐇𝐀𝐌𝐀𝐍𝐈 ya ardhi.ukipanga, ukipima na ukamiliki kisheria ardhi yako inapanda thamani kwa kuwa umiliki wako unatambulika 𝐊𝐈𝐒𝐇𝐄𝐑𝐈𝐀.

5)Kuongeza 𝐔𝐒𝐀𝐋𝐀𝐌𝐀 katika 𝐀𝐑𝐃𝐇𝐈 yako, hivyo kuzuia mtu yeyote kujimilikisha au kufanya shuguli yeyote katika ardhi yako bila ridhaa yako.

𝐊𝐀𝐑𝐈𝐁𝐔𝐍𝐈 𝐒𝐀𝐍𝐀 𝐒𝐔𝐑𝐕𝐄𝐘𝐄𝐃 𝐏𝐋𝐎𝐓𝐒 𝐂𝐎 𝐋𝐓𝐃
Ofisi zipo MWANGA TOWER floor ya 13
Kwa mawasiliano zaidi call/WhatsApp………………………..